Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TPA Tanga yajipanga kushawishi wamiliki wa Meli

Ijumaa , 30th Dec , 2022

Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA mkoa Tanga imesema kuwa imeandaa mikakati ya kupunguza gharama kwa muda maalumu (Low Cost) ili kuwavutia wateja na kufanya mazungumzo ya kuwashawishi wamiliki wa meli kuanza kuleta meli kubwa bandari ya Tanga badala ya kutumia bandari jirani. 

Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha

Hayo yamebainishwa na Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha wakati waandishi wa habari za kiuchumi, biashara na uwekezaji walipotembelea bandari hiyo na kujionea maboresho yanayoendelea katika bandari hiyo.

Meneja Mrisha amesema serikali kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), inatekeleza mradi huo mkubwa wa kimakakati wa maboresho makubwa katika bandari ya Tanga ili iweze kuchangia kikamilifu katika kukuza pato la Taifa kwa kuhudumia wateja wa ndani na nchi jirani ambazo zinategemea bandari za Tanzania kusafirisha bidhaa kutoka na kwenda nje ya nchi. 

"Mikakati yetu ya kimasoko baada ya kukamilika kwa ujenzi huu ni pamoja na kuitangaza bandari ya Tanga kwa kutumia vyombo vya ndani kama Radio na luninga na kuonyesha makala maalumu nje ya nchi kwa kutumia watumishi wa bandari waliopo nchi tunazohudumia, pamoja na Balozi zetu nchi mbalimbali kuitangaza bandari," amesema Mrisha. 

Kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali katika mradi wa maboresho ya bandari hiyo mradi huo utakapokamilika utakuwa na faida mbalimbali ikiwemo uwezo wa bandari ya Tanga wa kuhudumia shehena utaongezeka kutoka tani  750,000 mpaka tani 3,000,000.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali