Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TRA yakusanya Trilioni 3.84, maombi 1950 yatajwa

Jumatatu , 8th Oct , 2018

Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), imekusanya kiasi cha jumla ya shilingi trilioni 3.84 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 sawa na ukuaji wa asilimia 5.32% ndani ya miezi 3, ikilinganishwa na shilingi trilioni 3.65 zilizokusanywa kipindi cha miezi hiyo kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Katika taarifa yake aliyoitoa leo mbele ya waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Elimu na huduma kwa mlipa kodi TRA, Bw. Richard Kayombo amesema fedha hizo zilizokusanywa zimetokana na ongezeko la walipakodi nchini, ndani ya kipindi cha mwezi Julai, Agosti na Septemba mwaka huu.

"Katika mwezi Julai tulikusanya trilioni 1.2 sawa na 9.2%, Agosti tulikusanya trilioni 1.27 sawa na 5.86% na Septemba tulikusanya trilioni 1.36 sawa na 1.65%, kodi zote hizi zimetokana na kuongezeka kwa walipa kodi, kulipa kodi kwa hiari kote nchini, kwani kama TRA tumekuwa tukiendelea na juhudi za kuhakikisha elimu ya ulipaji kodi inawafikia wananchi." amesema Kayombo.

Aidha akitoa takwimu juu ya zoezi la kutoa msamaha wa riba na adhabu kwa wale wanaostahili kwa malimbikizo ya kodi za nyuma Bw. Kayombo amesema, "mpaka sasa tumepokea maombi 1950 kwa walipa kodi kote nchini yanayojumuisha riba na adhabu ya shilingi bilioni 185.4, ambapo maombi mengi yamejibiwa huku tukiendelea kuyafanyia uvumbuzi yale ambayo yamebaki na tunawaomba walipa kodi wajitokeze kwani mwisho wa zoezi hili ni Novemba 30, mwaka huu".

Pia Kayombo amewaonya wale wote wanaofanya udanganyifu katika risiti za 'EFD' kuacha kugushi na kutoa risiti zisizo halali, huku akisema tabia hiyo imesheheni maeneo ya biashara mitaa ya Kariakoo, jijini Dar es salaam na kuahidi kuwafikisha mahakamani wale wote watakaobainika na uvunjaji wa sheria hiyo.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya