Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wafanyabiashara wa Tanzania kuwekeza Slovakia.

Jumapili , 26th Feb , 2023

Balozi wa Heshima wa Jamhuri ya Slovakia nchini Tanzania Mhe. Moustafa Khataw ametoa wito kwa wafanyabiashara wa Tanzania kuchangamkia fursa za kiuchumi kwa kushirikiana na wenzao wa nchi hiyo ambao wameonesha nia ya dhati ya kutaka kuwekeza Pamoja kufanya biashara na Tanzania.

Khataw ameyasema hayo katika wakati wa kongamano la uwekezaji na biashara la Umoja wa Nchi za Ulaya lililofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.

Amesema Slovakia, iliyojipatia uhuru wake Januari 1, 1993 baada ya kuvunjika kwa amani umoja wake na Czechoslovakia, ni nchi iliyoendelea na yenye uchumi wa hali ya juu wa kipato, ikishika nafasi ya 45 katika Kielelezo cha Maendeleo ya Kibinadamu.

“Kuvurugika kwa uchumi katika maeneo yao kutokana na mgogoro wa Urusi na Ukraine wenzetu hawa wa Slovakia wameamua kugeukia Afrika kuendeleza shughuli zao za biashara na uzalishaji na wamevutiwa mno na Tanzania kwa kuwa nchi ya amani na vivutio vyema vya uwekezaji”, amesema Khataw.

Khatawa amesema jumla ya makampuni 18 toka Slovakia yamehudhuria kongamano hilo la biashara la EU lililofunguliwa siku ya Alhamisi na Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango na kufungwa siku ya Ijumaa na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Pamoja na mambo mengine, amesema makampuni kadhaa yamedhamiria kuwekeza nchini Tanzania katika Nyanja mbalimbali, ikiwemo ujenzi wa nyumba bora za bei nafuu na uzalishaji wa mbolea halisi.

Amesema Slovakia pia ni wazalishaji wakuu wa magari kwa kila mtu duniani, ambapo ilitengeneza jumla ya magari milioni 1.1 mwaka wa 2019, ikiwa ni asilimia 43 ya jumla ya pato lake la kiviwanda.

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali