Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

WATAKAOTOROSHA MADINI WANAITAFUTA JELA

Jumatatu , 3rd Oct , 2022

Waziri wa Madini Dkt. Dotto Biteko amewaonya wachimbaji wa Dhahabu wanaotorosha madini hayo kwa kupunguza thamani yake kukiona cha moto kwani serikali imejenga miundombinu ya kuuzia dhahabu na imepunguza gharama ya tozo zilizokuwa zinawafanya wachimbaji wakwepe masoko ya ndani.

Waziri wa Madini Dkt. Dotto Biteko

Dkt. Biteko ameyasema hayo wakati anazindua maonesho ya tano ya Teknolojia ya uwekezaji kwenye sekta ya Madini yaliyofanyika viwanja vya bombambili mkoani Geita na kuwaonya wachimbaji na wauzaji wa Dhahabu kuacha mara moja utoroshaji huo.

"Umetoka kwenye utoroshaji wa kubeba Dhahabu ukaificha ukaenda kuuza mahali pengine umekuja utoroshaji mwingine wa kisayansi, unashusha purity ya Dhahabu, kama Dhahabu ina 90% basi unashusha inakuwa 87% unaiba 3%, nataka niwaambieni wanaofanya jambo hili mambo mawili wanayatafuta, wanatafuta a wanatafuta umaskini, sheria ya madini inaeleza dhahiri mtu yeyote atakaefanya kitendo cha namna hiyo kwanza madini hayo yaliyofanyiwa ujanja yatataifishwa pamoja na vyombo vyote vibavyotumika kuyasafirisha na utakapopelekwa mahakamani utapigwa faini mara tatu ya thamani ya madini hayo," amesema Waziri Biteko. 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigella anasema kupitia maonesho hayo wamejiandaa kutoa nafasi kwa wafanyabiashara ambao wapo tayari kuweka miundombinu ya kudumu kwenye viwanja hivyo.

"Tumejipanga kuanzia mwakani tunataka tuweke utaratibu mzuri wale ambao watataka kuweka miundombinu  ya kudumu tuweze kugawa  maneneo waweze kuyajenga hapa ili shughuli za maonesho zisibaki kufanyika kwa mwaka mara moja peke yake tuweze kuwa na shughuli za utangulizi kabla ya kuwa na shughuki za maonesho zinazofanyika mwezi wa nane au mwezi wa tisa",amesema Martine Shigela. 

Baadhi ya washiriki wa maonesho hayo wanasema waliona umuhimu wa kushiriki ili waweze kutoa Elimu kwa wananchi juu ya taasisi zao.

 

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali