Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

ACT wataja sababu za kumchagua Othman Masoud

Jumanne , 2nd Mar , 2021

Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, amesema kuwa waliamua kumpendekeza Othman Masoud, awe mrithi wa Maalim Seif, kwa sababu ya misimamo yake na uwezo wake uliojipambanua kuhusu maslahi ya Zanzibar na ni mtu ambaye hakutaka sifa za kisiasa.

Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud

Kauli hiyo ameitoa hii leo Machi 2, 2021, kwenye kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio, na kuongeza kuwa mchakato wa kupendekeza jina haukuwa rahisi kwani walihitaji mtu ambaye angeweza kuvaa viatu vya Maalim Seif, na kwamba kati ya wanasiasa wote wa Zanzibar hakuna ambaye ameweza kumtilia shaka Othman Masoud.

"Othman Masoud ukiwachambua wanasiasa wa Zanzibar hakuna hata mmoja ambaye atamtilia mashaka katika misimamo yake juu ya maslahi ya Zanzibar na yeye ameshawahi kuonesha misimamo mikubwa isiyotarajiwa pale maslahi ya Zanzibar yanapotishiwa na wakati akiwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar alichukua msimamo wa kuipinga Katiba inayopendekezwa katika vifungu visivyozingatia maslahi ya Zanzibar," ameeleza Ado Shaibu.

Jana Februari Mosi, 2021, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi, alimteua Othman Masoud, kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar na ameapishwa hii leo.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali