Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Afisa aliyekamata bangi milimani, ateuliwa na Rais

Jumatatu , 6th Jul , 2020

Rais Magufuli amempandisha cheo aliyekuwa Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya nchini, Bw. James Kaji na kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo.

Rais Magufuli akimuapisha Kamishna James Kaji

Amefanya uteuzi huo leo, Ikulu Chamwino Jijini Dodoma alipokuwa akihutubia baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali wakiwemo Wakuu wa Mikoa, Katibu Tawala wa Mkoa pamoja na Wakuu wa Wilaya aliowateua hivi karibuni, ambapo amemuapisha afisa huyo kuanza kuitumikia kazi yake.

Rais Magufuli amesema amemteua Bw. James Kaji kutokana na kuridhishwa na kazi nzuri anayoifanya, baada ya kutembelea Wilayani Meru na kukamata magunia ya bangi na kuyateketeza.

"Jana nilikuona wa madawa unapita kwenye milima kule, unapita kwenye mji unakuta magunia ya bangi, IGP nataka Mkuu wa Polisi wa Meru aondolewe na Afisa Usalama wa wilaya hiyo naye aondolewe. Wewe Kamishna wa Madawa ya Kulevya leo mimi nakuthibitisha umefanya kazi nzuri. Nataka mambo yaonekane", amesema Rais Magfuli.

"Madawa ya Kulevya mpaka mtu atoke Dar es Salaam ndiyo akayaone wakati hapo kuna Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, OCD?. Kila mmoja afanye majukumu yake, najisikia raha kufanya kazi na watu wachapakazi", ameongeza.

 

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini