Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ajali yaua 19 Singida

Jumanne , 29th Apr , 2014

Watu 19 wa kijiji cha Utaho wilayani Ikungi wamepoteza maisha wakiwemo askari wanne wa jeshi la polisi, baada ya kugongwa na basi la summry

SACP Godfrey Kamwela, Kamada wa polisi mkoa wa Singida

Watu 19 wa kijiji cha Utaho wilayani Ikungi wamepoteza maisha wakiwemo askari wanne wa jeshi la polisi, baada ya kugongwa na basi la summry wakati wakiwa wanatoa msaada wa kumpakia marehemu kwenye gari la polisi aliye gongwa na gari kubwa ambalo halikufahamika mara moja.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo kamanda wa jeshi la polisi mkoani singida SACP Geofrey Kamwela, amesema  ajali hiyo ambayo imetokea katika kijiji cha Utaho Wilayani Ikungi, ilianza kwa lori kumgonga mtembea kwa miguu na kufariki papo hapo.

SACP  Kamwela amesema wakati askari na wananchi wakifanya utaratibu wa kuitoa maiti hiyo na kuiweka kwenye gari la polisi, ndipo lika fika basi  la Sumry lenye usajili wa namba T 799 BET na  ghafla likatoka nje ya barabara na kuwagonga watu waliokuwa wamefika eneo hilo na kuwakanyaga na kusababisha vifo vya watu hao. 

Kwa upande wake kaimu mganga mkuu wa hospitali ya mkoa wa singida  Dkt Musa Kimala ,amesema awali wamepokea maiti 14 na nyingine tano zilikuwa zipo katika hospita ya misioni ya Malkia wa ulimwengu Puma  na majeruhi wawili ambao wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa singida  wamepatiwa matibabu na wengine sita wanapatiwa katika hospitali ya mision ya Malkia wa ulimwengu puma.

Wakielezea baadhi ya watu walio shuhudia ajali hiyo akiwemo mchungaji Adulile Mbwile ambaye alikuwa abiria wa basi la Sumry  amesema waliona gari la polisi likiwa barabarani na walipotaka kulipita upande wa kulia, wakaona kuna gari lingine linakuja ndipo dereva alipoamua kulipitisha basi upande wa kushoto na kuwapitia watu ambao walikuwa nje ya barabara 

Ajali hiyo ambayo ni ya kutisha na kusababisha vifo vya watu wengi kwa mara moja EATV imeshuhudia kuona miili katika eneo la ajali ikiwa vichwa vimepasuka, miili imevunjikavunjika na baadhi ya maiti  zimetengana vichwa na miiili.

Ajali kama hiyo mbaya  kwa mwaka huu ni ya pili kutokea, ambapo mwanzoni mwa mwaka huu basi dogo aina ya Noah iligongana na lori na kusababisha vifoo vya watu 13 wilayani Ikungi

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali