
Aliyekuwa Rais wa Afghanistan, Ashraf Ghani
Ghani aliondoka ghafla nchini Afghanistan wakati wanamgambo wa Taliban walipokuwa wakiendelea kuingia kwenye mji mkuu mnamo Agosti 15 mwaka huu.
"Niliondoka kwa kushawishiwa na usalama wa Ikulu, ulionishauri kuwa kuendelea kuwepo kulihatarisha kutokea kwa mapigano mitaani na katika barabara za mji kama ilivyotokea wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka ya 1990," ameeleza
Aidha, Ghani ameongeza kuwa hakuwa na nia ya kuwaacha watu wake lakini ilikuwa ndio njia pekee iliyosalia.