Anastazia Mashaka, aliyeshuhudia mama yake akichomwa visu 16 na baba yake
Akiongea kwenye kogamano la wanawake lililofanyika mjini Geita, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Geita Rehema Mtawala, amesema mtoto huyo Januari alifukuzwa shule kutokana na kukosa ada hivyo serikali ikaamua kumuhamishia shule ya sekondari ya serikali ya Ihanamilo.
Kutokana na mtoto huyo kukosa mahitaji muhimu Halmashauri ya Mji kupitia Mkurugenzi Zahra Michuzi, wameamua kumchukua na kumlea binti huyo ili aepukane na changamoto za kimaisha anazozipitia tangu mama yake afariki na baba yake akiwa bado mahabusu.
Kwa upande wake mtoto huyo amewashukuru watu wote walioungana nae katika kipindi kigumu mpaka alipohamishiwa shule ya serikali.




