Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Amuuwa mwenzake kisa alinyimwa supu ya kuku

Alhamisi , 26th Sep , 2019

Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara, imemuhukumu adhabu ya kifo mkazi wa Kata ya Chikonji, Manispaa ya Lindi, Mohamedi Hassani Omari (45), baada ya kukutwa na hatia ya mauwaji ya kukusudia dhidi ya Andrew Ndemba (Mtanzania) kisa alimnyima supu ya kuku.

Hukumu hiyo imetolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Paul Ngwembe, baada ya ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka kuthibitishwa bila kuacha Shaka yeyote.

Jaji Ngwembe akitoa hukumu katika kesi hiyo namba 48/2016, kupitia kifungu cha Sheria namba 196 kanuni ya adhabu sura ya 16/2002, alimuhukumu Mohamedi Hassani Omari (45), adhabu ya kunyongwa hadi kufa.

Mwanzoni ilidaiwa mahakamani hapo na Mwanasheria wa Serikali, Emmanuel John, kuwa Mohamedi Hassani Omari alifanya mauwaji hayo Aprili 07/2016 usiku,baada ya Andrew Ndemba maarufu (Mtanzania) kukataa kumnunulia Supu ya kuku.

Alisema siku hiyo ya tukio, Mohamedi Hassani Omari akiwa ameongoza na mpenzi wake, walifika nyumbani kwa rafiki yao na walikumkuta marehemu akiwa anakunywa supu ya kuku, na kuomba amnunulie lakini alijibiwa hana fedha.

Wakili John ameeleza kuwa majibu hayo, yalimchukiza mshitakiwa Mohamed ndipo mzozo ulipoanza huku akimpa kauli za vitisho kuwa atamuonyesha, ambapo marehemu alilipiga teke sufuria la supu, kisha kuondoka eneo lile akiwa na rafiki yake Issa Abdallah.

Alisema wakiwa wanaelekea nyumbani kwao, mshitakiwa alichukuwa panga na kwenda kuwavizia njia ambayo walikuwa wakiitumia kupita na walipokaribia eneo alilosimama mshitakiwa aliwasimamisha, na kutekeleza azmio lake la kuuwa.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali