Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Askari aliyemuokoa mtoto shimo la choo atoa ahadi

Jumamosi , 23rd Mei , 2020

Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wilayani Ngara mkoani Kagera, Denice Minja ambaye alimwokoa mtoto katika shimo la choo cha shule ya msingi Murgwanza wilayani humo, ameahidi kumlea mtoto huyo katika maisha yake yote.

Askari wa Zimamoto wilayani Ngara, Denice Minja

Akizungumza baada ya kuvishwa cheo kipya rasmi na Kamanda wa Zimamoto mkoa wa Kagera Hamis Dawa, askari huyo amesema kuwa amekwishafanya mazungumzo na mke wake na wote wamekubaliana kumlea, pia amefuatilia idara ya ustawi wa jamii na kuambiwa mtoto akiruhusiwa kutoka hospitali aende kwa ajili ya kupewa fomu ya kujaza ili akabidhiwe. 

Askari huyo amesema aliposikia sauti ya mtoto yeye kama mzazi alihisi uchungu na kuamua kujitoa mhanga kuingia katika shimo hilo lenye urefu wa mita 30 na baada ya kumfikia mtoto huyo mwenye jinsia ya kike alikuta amefungwa mdomo kwa khanga na kuwa hilo linathibitisha kuwa mhusika alilenga kumuua. 

Akimvisha cheo kipya cha Koplo kutoka cha zamani cha Konstebo, kamanda wa Zimamoto na Uokoaji mkoa wa mkoa wa Kagera, Inspekta Hamis Dawa amesema kuwa askari huyo amepandishwa rasmi cheo jana na Kamishna Jenerali wa jeshi hilo, John Masunga kutokana na ujasiri wake wa kuingia katika shimo kumwokoa mtoto huyo.

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP