Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baada ya matukio ya mauaji, mengine yaibuka Mbeya

Jumatatu , 18th Feb , 2019

Baadhi ya wananchi wanaoishi katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbalizi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, wameingiwa na hofu baada ya kuibuka wimbi la ubakaji wa watoto unaotekelezwa na watu wasiojulikana huku vitendo hivyo vikihusishwa na imani za kishirikina.

Picha hii haihusiani na habari

Mpaka sasa watoto wanne wamenusurika kubakwa huku wabakaji hao wakifanikiwa kumbaka mtoto mmoja ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Mapinduzi alipokuwa akitoka akitoka shuleni jioni.

Diwani wa eneo hilo, Kasmine Mwangomale amewataka watumishi wa kiroho wakiwemo wachungaji kukiweka kitongoji hicho mikononi mwa Mungu ili matukio kama hayo yaweze kukoma, huku akieleza kuwa mara nyingi maiti zinaokotwa zikiwa zimetelekezwa sehemu mbalimbali kwa muda mrefu.

Naye Mchungaji wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Vumilia Mwasenga, ameeleza kuwa Februali 17 mwaka huu walipokuwa kanisani wanaendelea na ibada, mtu mmoja alitaka kuwabaka watoto watatu wenye kati ya miaka 12 na 13.

Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Mbeya, Debora Hokololo, amesema Jeshi la Polisi litafanya kila namna kuhakikisha wahusika wa matukio hayo wanakamatwa na kushughulikiwa na kuwataka wazazi na walezi kuimarisha ulinzi wa watoto wao kwa kuhakikisha hawawaachi peke yao majumbani ama kuwatuma peke yao kwenda madukani nyakati za usiku.

"Ina maana mnataka tuwalinde watoto wetu kama yanayotokea kule Njombe?, kule wameua na sisi tunaanza kubaka. Haya ni matunda ya kuwasikiliza waganga, naagiza kesi zote za matukio haya zifunguliwe", amesema OCD wa wilaya ya Mbeya, Debora Hokololo.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya