Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Barabara, Songea – Makambako km 295 kujengwa upya

Jumatatu , 18th Mar , 2024

Serikali ya awamu ya sita kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa miundombinu ya barabara na madaraja mkoani Ruvuma inaimarishwa ili kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji wa watu na bidhaa mbalimbali kwa ajili ya kuinua Uchumi.

Barabara ya Songea – Makambako km 295

Katika kipindi cha miaka mitatu ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali imeendelea na utekelezaji wa Miradi ya mikubwa ya Ujenzi wa Barabara, Madaraja na na Viwanja vya ndege, ikiwa ni pamoja na barabara ya Mbinga – Mbamba bay km 66 ambayo imekamilika na Ujenzi wa Daraja la Ruhuhu lenye urefu wa mita 98.01 ambalo linaunganisha Wilaya za Nyasa Mkoani Ruvuma na Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe.

Akizungumza na Waandishi wa Habari tarehe 14 Machi 2024; Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma Mha. Salehe Juma Mkwama amesema vile vile Serikali imefanya Ukarabati na Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege Songea na inaendelea na Ujenzi wa kiwango cha lami katika Barabara ya Kitai -Lituhi - Ndumbi km 95. 3; inayoelekea Bandari ya Ndumbi, ambayo pia inatumika kusafirisha Makaa ya Mawe.

Amesema kutokana na kutumika muda mrefu na hivyo kuchakaa; Serikali ipo mbioni kujenga upya barabara ya Songea – Makambako km 295 na imekusudia kujenga Daraja la Mitomoni, Barabara ya Likuyufusi hadi Mkenda km 124 ikijumuisha ujenzi wa Daraja la Mkenda linalounganisha nchi ya Tanzania na Msumbiji katika mto Ruvuma na Ujenzi wa Barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo – Kitanda – Lumecha km 512 ambayo inaunganisha mikoa ya Ruvuma na Morogoro.

Mha. Salehe amesema pia Serikali kupitia TANROADS imefanya usanifu katika Barabara za Mbamba bay – Lituhi km 112.4, barabara ya Mtwarapachani – Nalasi – Tunduru km 300, Barabara ya Unyoni – Maguu – Kipapa km 25, Barabara ya Nangombo – Chiwindi km 40, na Barabara ya Madaba – Mundindi (Liganga) – Mkiu km 35.

Ameongeza kuwa TANROADS Mkoa wa Ruvuma inasimamia mizani 4 kwa ajili ya kudhibiti magari yasizidishe uzito na kuharibu barabara, ambazo zipo katika vijiji vya Lipokela kwenye barabara ya Songea – Mbinga, Luhimba kwenye barabara ya Songea – Lukumburu, Sisi kwa sisi kwenye barabara ya Tunduru – Lumesule na Kijiji cha Buruma katika barabara ya Mbinga – Mbamba Bay.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma