
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Benjamin Kuzaga na timu yake wakikagua barabara ya mchepuko katika eneo hilo
Kamati ya ulinzi na usalama mkoani humo, imezindua barabara hiyo ambayo itasaidia kupunguza foleni na kukabiliana na ajali za mara kwa mara kwenye eneo la Inyala .
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga, amesema ujenzi wa barabara ya mchepuko umekamilika sasa wataanza kuwakamata na kuwachukulia hatua za kisheria madereva wote watakaokiuka utaratibu uliotolewa na kikosi cha usalama barabarani.