Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bodi ya Mikopo Serikali za Mitaa yaelemewa

Alhamisi , 27th Oct , 2016

Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa inakabiliwa na maombi makubwa ya mikopo kutoka katika halmashauri zake hadi kufikia shilingi bilioni 48.8 ikilinganishwa na shilingi bilioni 9.2 zinazotolewa sawa na asilimia 18.9.

George Simbachawene - Waziri wa TAMISEMI

 

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa bodi mpya ya mikopo mjini Dodoma leo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi, George Simbachawene, amesema, upo umuhimu wa kuangalia namna bora ya kuongeza mtaji ili kuboresha huduma ya bodi hiyo.

Mh. Simbachawene amesema ili kukabiliana na changamoto hizo lazima baadhi ya hatua zianze kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na halmashauri  zinazodaiwa kutakiwa kulipa madeni kupitia makato ya benki.

Amesema halmashauri zitakazoidhinishiwa mikopo lazima marejesho yake yafanyike kulingana na makubaliano ya mkataba uliopo huku akiitaka bodi mpya kuhakikisha marejesho yanafanywa kwa wakati.

Pia Simbachawene aliwakumbusha majukumu wajumbe wa bodi ya mikopo kuwa pamoja na kuwajibika kuzisaidia halmashauri kutimiza malengo yao pamoja na upelekaji madaraka na majukumu zaidi kwa wananchi ambako kunahitajiwa fedha na nyenzo  zaidi za kufanyia kazi.

Amesema majukumu mengine ni umuhimu wa kuwezesha halmashauri kupata mapato ya ziada pamoja na kutoa msaada wa fedha kwa serikali za mitaa kwa njia ya ruzuku kwa niaba au faida ya serikali za mitaa.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi