Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Florens Luoga
Taarifa hiyo imetolewa leo Oktoba 28, 2021, na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Florens Luoga, na kusema kwamba fedha hizo wakati mwingine huwekwa kwenye mwili wa mtu aliyeloa jasho na kusema vitendo hivyo vinasababisha fedha hizo kuchakaa na kuiongezea serikali gharama kubwa ya kuchapisha noti mpya.
Mbali na hayo Benki Kuu imewashauri washiriki katika matukio yote ambayo yanahusisha matukio ya fedha, kuandaa vyombo maalum vya kuwekea fedha hizo badala ya kufanya vitendo ambavyo havikubaliki.
Hivi karibu Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi, alitoa onyo kuhusu watu wanaotunza fedha kwa kuzitupa chini kwani ni kinyume cha sheria.






