Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

CCM yawaonya wanaotangaza nia ya kuwania urais

Ijumaa , 18th Jul , 2014

Kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi nchini Tanzania CCM imewatahadharisha wanachama wake walioonesha nia ya kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kuwa wanaweza wakapoteza sifa za kugombea nafasi hiyo.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama tawala nchini Tanzania CCM, Nape Nnauye.

Wanachama na makada hao wanaweza kupoteza sifa hiyo iwapo hawatazingatia katiba, Kanuni na taratibu za chama zinazosimamia masuala hayo.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jijini Dar es salaam juu ya maadhimio ya kamati kuu ya chama hicho iliyokutana chini ya mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye amesema kumekuwa na baadhi ya wanachama wa CCM ambao wanatangaza nia ya kugombea urais kupitia chama hicho bila ya kufuata taratibu.

Aidha Nape amesema wale ambao wameshapewa adhabu na kamati kuu kutokana na kukiuka baadhi ya taratibu za chama kwa suala hilo, kamati kuu ya usalama na maadili ya CCM itafanya mapitio ya mwenendo wao ya utekezaji wa adhabu hiyo na kama watabainika hawatekelezi ipasavyo wataongezewa adhabu.

Makada ambao mwenendo wao utaangaliwa ni pamoja Bernard Membe, Edward Lowassa, Frederick Sumaye, William Ngeleja na Stephen Wassira ambao wanaotwa kuwa katika kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu wa Mwakani.

Kwa mujibu wa Nape, makada hao wa CCM walipewa miezi kumi na mbili ya uangalizi, muda ambao wanasiasa hao walitakiwa waonyeshe nidhamu kwa kufuata taratibu, sheria na miongozo ya chama ikiwa ni pamoja na kutofanya kampeni za mapema za kuwania urais.

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini