Alhamisi , 23rd Feb , 2023

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limebaini kwamba, uzembe na kutojali alama za barabarani kwa dereva wa gari ndogo aina ya Toyota Avanza ndiyo chanzo cha ajali iliyohusisha basi la mwendokasi na gari hilo jana Februari 22, 2023, maeneo ya Kisutu jijini humo.

Basi la mwendokasi lililopata ajali

Gari hiyo yenye namba T978 DHZ ilisababisha ajali hiyo wakati dereva wake akitoka Mnazi Mmoja kuelekea mzunguko wa DTV kutochukua tahadhari wakati anakatisha barabara kubwa ya Morogoro. 

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, amesema watu wanne wamelazwa na kuendelea kupata matibabu katika Hospitali Taifa Muhimbili akiwemo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Ismail ni mtembea kwa miguu, Jumbe Mohamed (38) dereva wa gari ndogo T978 DHZ aina ya Toyota Avanza, Shukuru Omari (32)abiria wa gari ndogo na Saidi Hasani (43) abiria wa gari ndogo.