Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chanzo cha moto uliounguza nyumba ya DED chatajwa

Jumamosi , 14th Nov , 2020

Kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu, ACP Richard Abwao, amesema kuwa moto ulioteketeza nyumba aliyokuwa akiishi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Meatu, Fabian Manoza, ulisababishwa na uwepo wa baadhi ya vifaa mbalimbali vya umeme vilivyokuwa vimechomekwa ikiwemo Friji.

Kamanda wa Polisi, mkoa wa Simiyu, ACP Richard Abwao.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Novemba 14, 2020, wakati akizungumza na EATV&EA Radio Digital, kuelezea tukio la moto uliounguza nyumba hiyo, tukio ambalo limetokea usiku wa kuamkia leo na wakati nyumba inateketea Mkurugenzi huyo hakuwepo nyumbani, bali aliyekuwepo ni mdogo wake.

"Nyumba yote imeteketea kwa moto, nje kulikuwa na gari nalo kidogo liungue ila lilivutwa, na chanzo cha moto mule ndani, waliacha vitu vikiwa vimechomekwa kwenye umeme, ikiwamo friji, chaji za simu na vingine, nadhani umeme ulicheza ikatokea shida," amesema RPC Abwao.

Aidha Kamanda Abwao ameongeza kuwa wakati wa tukio hilo, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji walifika eneo la tukio, lakini wakashindwa kuuzima moto huo, "Mule ndani moshi mzito ulikuwa umetanda sana, hivyo zimamoto hawakuingia na hakuna madhara yoyote kwa binadamu na uchunguzi unaendelea ili kukibaini hasa kiini cha moto huo".
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali