Gari ndogo aina ya Noah iliyokuwa imebeba abiria,ikiwa imepondeka vibaya.
Ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia Machi 23, 2020, huku chanzo kikielezwa kuwa ni kufeli kwa breki ya Lori na kupelekea vifo vya watu wanne papo hapo na mmoja kufariki wakati akipatiwa matibabu hospitalini.
Akizungumza katika eneo la tukio Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Wilbroad Mutafungwa, ameeleza kuwa gari hiyo ndogo ilikuwa imebeba abiria kutoka Dumila kuelekea Gairo na kwamba Jeshi la Polisi linaendelea kumtafuta dereva wa Lori kwani alikimbia.