Akiongea leo jijini Dar es Salaam Waziri wa Jinsia na Makundi Maalum wa (DARUSO), Rose Makupa amesema zaidi ya matukio 120 ya kesi yameripotiwa huku kesi 11 zikiwa zimefikishwa mahakamani na kesi tano pekee zikiwa zimetolewa hukumu jambo linalohusishwa na viongozi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha wanafunzi wenye albinism wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Perpetua Senkoro amesema vyombo vya sheria na usalama vimekuwa havifanyi upelelezi wa kina ili kuwatia hatiani watuhumiwa.