Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dereva bodaboda auawa Lindi

Jumanne , 28th Mar , 2023

Watu wawili ambao hawajajulikana hadi sasa wamemshambulia na kumsababishia kifo kijana mmoja anayefahamika kwa jina la Zulkif Hemedi ambaye ni dereva bodaboda mkoani Lindi

Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoani Lindi  Pili Mande amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo ambapo amesema vijana hao wawili walimhadaa dereva bodaboda huyo na mwishowe kumjeruhi kwa kitu chenye ncha kali na kumsababishia kifo

Taarifa za wananchi na viongozi katika kijiji cha Nangaru zinasema, Bodaboda huyo ambaye kwa asili ni mzaliwa wa Kijiji cha Nangaru, alifuatana na abiria hao wawili ambao alielekea nao upande wa mashambani, lakini baada ya mda mfupi alifanikiwa kuwapigia simu rafiki zake aliowasabahi kijiweni na kuwataarifu kuwa, abiria wake wamemgeuka na kumshambulia vibaya kiasi cha kupoteza fahamu.

Inasemekana kuwa, walipomshambulia na kumwacha chini, walifanikiwa kumpora simu kubwa na kumwacha marehemu na simu ndogo ambayo hawakufahamu kama aliificha mfukoni. 

Baada ya kupiga simu na kuomba msaada, wasafirishaji wenzake walitoa taarifa kijijini na kufanya msako mkubwa hadi kijiji jirani ambapo  walifanikiwa kuzuia barabara lakini jitihada za kuwakamata wahalifu hao iligonga ukuta, kwani walifahamu njama ya wanakijiji na kuamua kuitelekeza pikipiki vichakani na kukimbia.

Jeshi la Polisi Mkoani Lindi linaendelea kufanya msako mkubwa ili kuwabaini wahalifu hao huku polisi wakiwataka Madereva bodaboda wote kuwa na umoja lakini pia kusoma alama za hatari mapema ili waweze kujilinda na kutoa taarifa wanapohisi wapo mashakani

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya