Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Diwani na wenzake mahakamani kwa tuhuma za mauaji

Jumanne , 6th Dec , 2022

Watu 14 akiwemo Diwani wa Kata ya Buzilasoga David Shilinde, Mwenyekiti wa CCM Kijiji cha Ikoni B William Nengo na Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Tiluloza Alphonce, wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza kwa tuhuma za mauaji ya mwanamke aitwaye Getruda Dotto.

Diwani na wenzake 13 walivyofikishwa mahakamani

Ni kesi namba 23 ya mwaka 2022 ambayo leo hii imetajwa katika Mahakama ya wilaya ya Sengerema mbele ya Hakimu Mfawidhi Tumsifu Barnabas, ambapo Mwendesha Mashtaka wa serikali Theophilius Lucas, ameiambia Mahakama hiyo kuwa upelelezi wake bado haujakamilika na kuomba ipangiwe tarehe nyingine.

Baada ya maelezo hayo ya Mwendesha Mashtaka Hakimu Tumsifu Barnabas, akaiahirisha kesi hiyo hadi Desemba 20 ya mwaka huu huku washtakiwa wakirudishwa rumande katika gereza la Kasungamile.

Inadaiwa kuwa mnamo Novemba 5, 2022, majira ya saa 2:00 asubuhi katika Kitongoji cha Ikoni B, Kata ya Buzilasoga wilayani Sengerema mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Getruda Dotto akiwa nyumbani kwake na watoto wake wawili ghafla alivamiwa na kundi la watu wakiwemo viongozi hao wakaanza kumshambulia kwa kutumia fimbo na marungu huku wakimtuhumu kuiba mihogo kwenye shamba la mwanakijiji mwenzake.

Inaelezwa kuwa mwanamke huyo alijaribu kujiteteana kusema shamba hilo aliachiwa na marehemu mume wake  lakini watu hao waliendelea kumshambulia na baadae wakamchoma moto na kupelekea kifo chake.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ