Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dkt Bashiru atoa maagizo kwa Nape na Kigwangalla

Jumapili , 6th Sep , 2020

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt Bashiru Ally, amemtaka mgombea Ubunge wa Jimbo la Nzega Vijijini Dkt Hamis Kigwangalla, kuacha kujibizana mitandaoni kuhusu mpira na badala yake, atumie muda huo kuweka vitu vitakavyomsaidia mgombea Urais wa chama hicho Dkt Magufuli kushinda uchaguzi.

Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally

Hayo yameelezwa hii leo Septemba 06,2020, kupitia ukurasa wa Twitter wa CCM, ambapo licha ya kutoa maelekezo hayo kwa Kigwangalla, pia ametoa maelekezo kwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama Nape Nnauye.

"Naona Dkt Kigwangalla yupo mitandaoni kujibizana na Mohamed Dewji mambo ya mipira, tupo kwenye uchaguzi, nataka nione ana-tweet na wafuasi wake namna Mwenyekiti na Mgombea Urais wetu atakavyoshinda, siingilii maisha binafsi, hakuna maisha binafsi unapokuwa mgombea wa CCM" amesema Bashiru.

Dkt Bashiru pia akatoa maelekezo haya kwa Nape, "Nimemuona Nape Ilemela, wakati Jakaya kikwete anakwenda Lindi Septemba 8, 2020 kuzindua, anatakiwa awe Lindi kumuandalia Mkutano,tutakuwa wakali kusimamia nidhamu, wagombea wa CCM wapo chini ya Kamati za Siasa, lazima wafuate maelekezo, sio kujiamulia binafsi" ameongeza Dkt Bashiru.

Mbali na hayo Dkt Bashiru ameongeza kuwa, "Hakuna Mgombea yeyote kutoka Jimboni kwake bila idhini ya Kamati ya Siasa ya Wilaya, tufuate ratiba za NEC na  Kamati za Siasa, tuwatafutie kura wagombea Udiwani na Mgombea Urais, tufafanue Ilani yetu tuliyotekeleza na kilichobaki, na kuhamasisha wananchi kupiga kura"

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali