Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dkt. Magufuli asisitiza kuboresha sekta ya Afya.

Jumanne , 29th Sep , 2015

Mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli amewaahidi wakazi wa Mkoa wa Iringa kuwatatulia kero mbalimbali ikiwemo kuanzisha kiwanda cha kusindika mbogamboga, kutatua kero ya maji pamoja na kuboresha sekta ya Afya.

Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Wananchi wa Iringa

Akizungumza kwa nyakati tofauti na Wakazi hao katika mikutano yake ya Ilula, Kalenga pamoja na Iringa Mjini Mh. Magufuli amesema moja ya mikakati yake na ya Chama cha Mapinduzi ni kuboresha Sekta ya Afya kwa kiasi Kikubwa.

Mh. Magufuli ameongeza kuwa wataboresha bima ya afya ili kila mwananchi aweze kupata matibabu kwa wakati na kwa uwiano sawa tofauti na ilivyo sasa ambapo hata dawa wakati mwingine wanaambiwa wakanunue madukani ya watu Binafsi.

Aidha Mh. Magufuli amefafanua madhila yaliyompata wakati wa Uwaziri wake akiwa anawatumikia Watanzania ikiwemo kulala site za ujenzi wa madaraja na kuumwa na mbu pamoja na kuanguka kwenye helkopta jijini Dar es salaam wakati wa mafuriko.

Mgombea huyo ameongeza kuwa yeye ni mtu anayechukua sana rushwa hivyo wafanyakazi wanaofanyakazi kwa mazoea basi waanze kubadilika sasa kabla ya kuingia madarakani kwa kuwa hatawavumilia watendaji wabovu hata kidogo.

Kwa upande wake waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi amewataka wale watendaji wanauza au kunyang'anya viwanja vya watu kwa ujanja ujanja basi kiama chao ni pindi Dkt. John Magufuli atakapoingia madarakani.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali