Jumatano , 26th Jan , 2022

Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango, ametoa siku 7 kwa Jeshi la Polisi likiongozwa na IGP Simon Sirro, kufanya uchunguzi wa mauaji ya watu watano wakazi wa Kata ya Zanka, kijiji cha Zanka jijini Dodoma yaliyotokea hivi karibuni.

Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, na kulia ni Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango

Dkt Mpango ametoa maagizo hayo hii leo Januari 26, 2022, mara baada ya kutembelea eneo lilipofanyika tukio hilo na kutoa pole kwa wafiwa.

Aidha Dkt. Mpango, amelielekeza jeshi hilo kufanya misako nchi nzima ili kuwabaini wote wanaojihusisha na vitendo vya mauaji kwani, Taifa limechafuliwa na vitendo hivyo vya kikatili na vya kinyama.