
Akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Kamanda Muslim amesema kuwa siku ya Krismasi mwaka huu ajali zilizotokea zimesababisha nusu tu ya vifo vilivyotokea mwaka jana.
“Disemba 25 siku ya Krismasi zilitokea ajali 10 tu nchi nzima na kusababisha vifo 5 na majeruhi 11, ukilinganisha na mwaka jana ambapo zilitokea ajali 14 na kusababisha vifo 10 na majeruhi 15”, amesema Kamanda Muslim.
Aidha kamanda Muslim amewataka madereva kuendelea kuwa waangalifu katika kipindi hiki cha sikukuu na kuzingatia sheria za barabarani.