Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Fahamu hii fursa kwa wafanyabiashara na vijana

Jumatano , 9th Oct , 2019

Wafanyabiashara, vijana na wananchi, wametakiwa kuchangamkia fursa kutoka kampuni ya Bima ya Jubilee Insurance, ili kusaidia kuweka kinga dhidi ya majanga yote yanayohusiana na pesa pamoja na hasara za kiuchumi katika uzalishaji.

Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Kampuni ya Bima ya Jubilee

Wito huo umetolewa leo Oktoba 9, 2019, jijini Dar es salaam na Mkuu wa Mauzo Kitengo cha Wateja wa Rejareja kutoka Jubilee Insurance Bw. Abdulrauf Suleiman, wakati wa mahojiano maalumu katika muendelezo wa kampeni ya Kibiashara Zaidi inayoendeswa na vituo vya East Africa Television na East Africa Radio, ambapo ameeleza kuwa wanatoa bima katika maeneo mbalimbali ikiwemo maisha, Magari, Afya na Kilimo.

“Mfano bima ya magari ambayo ni kinga anayopatiwa mteja kusaidia kuokoa matumizi ya fedha endapo chombo hicho cha usafiri kitapata ajali ya kugongwa au moto ambazo zimegawanyika katika makundi mawili bima kubwa na ndogo”.

Amesema kuwa kampuni hiyo ambayo imedumu kwa kipindi cha miaka 30, imefanikiwa kutwaa tuzo nne ambazo zinadhihirisha uwezo wake katika utoaji huduma katika jamii, huku akiwataka wateja wafahamu umuhimu mkubwa wa kuweka kinga katika maeneo tajwa, ili kusaidia kuokoa hasara katika uzalishaji na uendelezaji wa shughuli za kiuchumi.

Amesema kuwa ni vyema wateja wakafahanu umuhimu mkubwa wa kuweka kinga, katika maeneo tajwa ili kusaidia kuokoa hasara katika uzalishaji na uendelezaji wa shughuli za kiuchumi.

Aidha amesisitiza uwepo wa fursa ya uwekezaji katika bima, ikiwa wao wamejikita katika utoaji wa huduma zaidi ya 30, hivyo kutoa nafasi za ajira kwa vijana kuweza kufungua ofisi ndogo ya bima kama wakala.

'Mpaka sasa mafanikio makubwa yamekuwepo   kutokana na utolewaji wa elimu kwa wafanyabiashara na watoa huduma mbalimbali katika jamii kuhusu kuweka kinga katika vitega uchumi vyao', ameeeleza.

Amemaliza kwa kutaja kuwa fursa ya uwekezaji katika bima ni kubwa ambapo mpaka sasa wao wamejikita katika utoaji wa huduma zaidi ya 30, hivyo kutoa nafasi za ajira kwa vijana kuweza kufungua ofisi ndogo ya bima kama wakala.
 

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil