Picha: Mvua ikinyesha
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mamlaka hiyo imeeleza kuwa mvua hizo zitanyesha kuanzia Januari 21 hadi Januari 25, 2020.
"Tunatoa tahadhari ya upepo mkali na mawimbi makubwa kwa baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Lindi na Mtwara, athari zinazoweza kujitokeza ni kuathirika kwa shughuli za uvuvi, ucheleweshwaji wa usafiri pamoja na kuanguka kwa majani na matawi madogomadogo ya miti." imeeleza taarifa hiyo.
Aidha mamlaka hiyo imewataka wananchi wa Mikoa hiyo, kuzingatia tahadhari iliyotolewa na wajiandae.