Mtoto Bennet Kiwelu
Dkt. August Mtui ambaye ni mjomba wa marehemu amesema kwa mujibu wa historia ya afya ya marehemu na ripoti za kitabibu, zinaashiria kwamba Bennet alikuwa na tatizo la kiafya ambalo limepelekea kifo chake baada ya kuzimia akiwa shuleni na baadaye kupoteza maisha Alfajiri Septemba 18 katika hospitali ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.
Taarifa zaidi usikose kutazama EATV SAA 1, ifikapo saa 1:00 jioni ndani ya East Africa TV.