Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Fimbo yetu ya mbali inaua Nyoka" - Mwangamilo

Jumatano , 27th Jul , 2022

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Arusha SP Solomoni Mwangamilo, amewaonya baadhi ya wamiliki na madereva wa mabasi yaendayo mikoani kuacha mara moja, tabia ya kushabikia mwendokasi kwani umekuwa ndiyo chanzo cha kupoteza maisha ya watu na atakayekamatwa atashughulikiwa kweli.

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Arusha SP Solomoni Mwangamilo

Kauli hiyo ameitoa hii leo Julai 27, 2022, wakati akiongea na madereva wa mabasi yaendayo mikoani katika stand kuu ya mabasi jijini Arusha, na kusema zipo taarifa kutoka kwa wananchi wema kuwa kuna baadhi ya wamiliki wanao washawishi madereva kwenda mwendo kasi na madereva hao kuyaendesha magari hayo kasi.

"Fimbo ya mbali ya kwetu polisi inaua Nyoka, kuna wamiliki wa mabasi wanashabikia mwendo, mtupe taarifa tutamfikia, na tutakachomfanya yeye ndiyo ataeleza tumemfanya nini, ajali zinaharibu system nzima za maisha ya watu, watu wamechoka kulia na kusononeka, nitakayemkamata nitamshughulikia zaidi ya kawaida," amesema SP Mwangamilo

SP Mwangamilo akawasisitiza madereva kuhakikisha wanafuata miiko ya uendeshaji na sheria za barabarani.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi