Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Geita Boys wapewa mbinu kufikia malengo kitaaluma

Jumanne , 19th Mar , 2024

Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana Geita (Geita Boys) kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao kutambua masomo sahihi wanayoyamudu na fani zinazoendana na masomo hayo katika soko la ajira.

Scholastica Kabonge -Ofisa wa masuala ya ulinzi shirikishi na usalama kutoka GGML (katikati), akiwapatia ushauri na uzoefu wake wa kitaaluma wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Geita kama sehemu ya Mpango wa GGML Mentorship Programme.

Mafunzo hayo yametolewa wiki iliyopita mkoani Geita na baadhi ya wafanyakazi wa GGML wakiwamo wanawake wanaounda kundi la GGM Ladies ikiwa ni mwendelezo wa maadhimisho ya sherehe za siku ya wanawake duniani.

 

GGML ladies imetoa mafunzo hayo ya siku moja kupitia program maalumu ya ushauri na usimamizi iliyopewa jina la (GGM Mentorship Program) kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi hao wa kidato cha kwanza hadi cha tano, kutambua uwezo wao kielimu na malengo waliyojiwekea katika kutimiza ndoto zao.

 

Akizungumza na wanafunzi hao, Ofisa wa masuala ya usafirishaji kutoka idara ya Rasilimali watu, Laila Mohamed alisema huu sio muda wa wanafunzi kufuata mkumbo katika kuchagua masomo ya kusoma na kufikia malengo yao kimaisha.

 

“Ili kufikia malengo ya kitaaluma, hiki sio kipindi cha kufuata mkumbo... kwamba ukisikia Juma amechukua biology na wewe unachukua mchepuo wa sayansi. Hiki ni kipindi cha kujitathmini na kujitafakari kwamba ni kitu gani unakimudu ili uchukue masomo sahihi kufikia lengo lako,” alisema.

 

Alisema wanafunzi wengi wamekuwa na changamoto ya kutokuwa na msimamizi au mshauri anayeweza kuwashauri namna ya kujinasua katika changamoto mbalimbali kitaaluma jambo ambalo GGML imeona ni vema kujaza nafasi hiyo.

 

Naye Joscar Rumanyika ambaye ni mhasibu kutoka GGML, aliwaonya wanafunzi hao kujiepusha na vitendo viovu vya uvunjifu wa maadili ili kutimiza malengo yao kitaalumu.

 

Joscar aliwataka wanafunzi hao kuwa na uthubutu na kujiamini kwamba hakuna kinachoshindikana ili kufaulu vema katika masomo yao.

 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wanafunzi hao kutoka Geita Boys, Leonard Martin na Daniel Stanslaus walisema mafunzo waliyopatiwa na GGML yamewasaidia kutambua namna ya kufikia malengo yao.

 

Martin (14) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili na mkazi wa Bwanga mkoani Geita, alisema alisema elimu hiyo inawawezesha kujiandalia maisha mazuri ya baadae.

 

Makamu Rais Mwandamizi wa AngloGold Ashanti-GGML - Kitengo cha Ubisa/ Ushirika Afrika, Terry Stron alisema program hiyo ya mentorship inalandana na malengo ya kampuni hiyo ya kuwekeza kwa vizazi vijavyo kwani kuwekeza kwa wanafunzi hao ni sawa na kuwekeza kwa jamii ya Geita ijayo.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ