
Hayati Emilio Mwai Kibaki
Msafara wa mazishi ya Hayati Rais Mstaafu wa Kenya Emilio Mwai Kibaki umeondoka asubuhi ya leo Jijini Nairobi kwa usafiri wa magari kuelekea Kaunti ya Nyeri Nchini Kenya.
Mwili wa Hayati Mwai Kibaki unatarajiwa kupitishwa katika Kaunti za Kiambu, Murang'a, Kirinyaga na baadae kufika Nyeri ili kuwapa fursa wakazi wa maeneo hayo kumuaga kiongozi wao.
Siku ya jana maelfu ya raia wa Kenya waliungana na viongozi mbalimbali wa Kenya na kutoka mataifa ya Afrika kwenye mazishi ya kitaifa kumwaga Mwai Kibaki, ambapo Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Philip Mpango alikuwa miongoni mwa viongozi walioshikiki katika hafla hiyo.
Hayati Mwai Kibaki, alifariki dunia Ijumaa ya Aprili 22, 2022 akiwa na umri wa miaka 90.