Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Ile ofisi ni ndogo nadhani Tulia haitaki"- Sugu

Alhamisi , 26th Nov , 2020

Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini, kupitia CHADEMA, Joseph Mbilinyi, amesema yeye hana mamlaka ya kumkabidhi ofisi mbunge wa sasa wa jimbo hilo kupitia CCM Dkt. Tulia Ackson, kwani ofisi aliyokuwa akiitumia, alikwisharudisha funguo kwa mamlaka husika na kwamba amuache na achape kazi

Kushoto ni aliyekuwa mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini kupitia CHADEMA, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu, na kulia ni mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Dkt. Tulia Ackson.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Novemba 26, 2020, wakati akizungumza na EATV&EA Radio Digital, na kuongeza kuwa hata yeye wakati anaingia kwenye hiyo ofisi zilizopo kwenye ofisi za ardhi, alikabidhiwa na halmashauri ya jiji na si yule mbunge aliyekuwepo kabla yake.

"Wewe umeshasikia wapi mbunge analia hajakabidhiwa ofisi, hakuna kitu kama hicho, aliyempa cheti cha ubunge ndiye angemwelekeza kwamba kinachofuata ni nini, afanye kazi aachane na Sugu", amesema Sugu.

Aidha Sugu ameongeza kuwa, "Yeye afuate utaratibu pengine hata sasa wamempa ofisi nyingine yeye ni mtu wa kujimwambafai, labda ofisi niliyokuwa naitumia mimi ni ndogo nadhani haitaki anatafuta 'justification' wampe ofisi kubwa zaidi kwa kusema Sugu hajanikabidhi ofisi, ofisi ni mali ya jiji".

Jumatatu ya Novemba 23, 2020, mbunge wa jimbo hilo Dkt. Tulia Ackson, wakati akizungumza na wanahabari nyumbani kwake, jijini Mbeya, alisema kuwa bado hajakabidhiwa ofisi aliyokuwa akiitumia mbunge Sugu na kwamba ataendelea na majukumu yake hawezi kumngoja kwani mlolongo ni mrefu.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa