Ijumaa , 6th Dec , 2019

Jengo la ghorofa 6 limeanguka nchini Kenya asubuhi ya leo, katika eneo la Embakasi jijini Nairobi, huku watu kadhaa wakihofiwa kukwama kwenye jengo hilo.

Jengo lililoanguka jijini Nairobi

Jengo hilo lipo Mtaa wa Tasia, Embakasi Mita chache kutoka Uwanja wa Ndege JKIA, huku chanzo cha kuanguka kwa ghorofa hilo kukitajwa ni mvua kubwa. 

Kwa mujibu wa taarifa za awali idadi ya watu wanaoshukiwa kunaswa ndani ya Jengo hilo bado haijulikani, huku shughuliza uokoaji bado zikiendelea kufanywa na vyombo vya ulinzi nchini humo.

Mpaka sasa hakujaripotiwa kifo chochote.

Tutaendelea kukupa taarifa  zaidi.