Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania,Simon Sirro
Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa hii leo ambapo IGP Sirro amesema kuwa kwa sasa hali iko shwari na bado wanaendelea na oparesheni mbalimbali ikiwemo dawa za kulevya na matuko ya unyang'anyi
Amesema hayo yamewezekana kutokana na ushirikiano uliopo kati ya vyombo vya usalama pamoja na wananchi wanaochukia uhalifu na wadau mbalimbali.
Aidha IGP Sirro ametoa wito kwa watanzania wote wenye mawazo chanya kwa nchi yao kushirikiana na vyombo vya usalama katika kubaini na kuzuia uhalifu.

