Jumanne , 28th Jan , 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameliandikia Bunge la Tanzania juu ya kupokea azimio la pongezi lililoafikiwa na Bunge hilo kwenye kikao cha 17.

Akisomabarua ya Rais kwenye ufunguzi wa Mkutano wa 18, Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai amesema Rais Magufuli analishukuru Bunge kwa kutambua mchango wake wa kuliletea maendeleo Taifa.

"Niendelee kuwahasa Wabunge na watanzania kwa ujumla tuendelee kuipambania nchi yetu, ili tuweze kufikia maendeleo yenye uchumi wa kati" amesema Spika Ndugai wakati akisoma barua ya Rais Magufuli