Akisomabarua ya Rais kwenye ufunguzi wa Mkutano wa 18, Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai amesema Rais Magufuli analishukuru Bunge kwa kutambua mchango wake wa kuliletea maendeleo Taifa.
"Niendelee kuwahasa Wabunge na watanzania kwa ujumla tuendelee kuipambania nchi yetu, ili tuweze kufikia maendeleo yenye uchumi wa kati" amesema Spika Ndugai wakati akisoma barua ya Rais Magufuli
#HABARI Spika wa Bunge Job Ndugai amesema Rais @MagufuliJP amepokea azimio la pongezi lililofikiwa na Bunge kwenye kikao cha 17, kufuatia mafanikio na mageuzi kwenye utendaji kazi wa Serikali na pia amelishukuru Bunge kwa kutambua mchango wake.#Bungeni pic.twitter.com/DnrKnn2dGQ
— East Africa Radio (@earadiofm) January 28, 2020