Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

JPM amwagiwa sifa

Jumamosi , 16th Dec , 2017

Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli imepongezwa kwa kuonyesha kwa vitendo utekelezaji wa sera ya elimu bure kwa wanafunzi nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwanafunzi Radhia Salumu wa shule ya sekondari Salma Kikwete leo alipohudhuria tamasha la  Coke5Seleket Concert linaloendelea katika Viwanja vya  Leaders Kinondoni Jijini  Dar es Salam, ambapo amesema kwamba ni matumaini yake elimu hiyo (bure) itaendelezwa mpaka vyuoni. 

"Ni vyema watanzania tumpongeze JPM kwa juhudi zake za kutoa elimu bure sio rahisi, naamini hii itafika hadi chuo kikuu " amesema.

Mbali na hayo mmoja wa wanafunzi kutoka shule ya sekondari Kambangwa aliyejulikana kwa jina la Ashura Iddi amesema hakuna njia ya mkato katika kutafuta elimu na kuwashauri wanafunzi wenzake  kutokata tamaa katika kuitafuta elimu ili wajikomboe katika janga la umasikini.

"Naamini katika elimu lazima uwe na uvumilivu ili  uweze kufanikiwa hakuna njia ya mkato katika kutafuta elimu. Sisi tunatakiwa kujiandaa katika maisha yetu ya baadae hivyo tujitahidi katika masomo, "amesema

Wanafunzi kutoka Maeneo Mbali Mbali ya Dar es Salama na maeneo ya jirani wamejitokeza na kujumuika kwa pamoja katika tamasha la Coke5Seleket Concert linaloendelea katika Viwanja vya  Leaders Kinondoni Jijini  Dar es Salama. 

Tamasha la Coke5Seleket Concert  limeandaliwa na Coca Cola ikishirikiana na East Africa LTD likiwa na lengo la kuwakutanisha wanafunzi na kusherehekea kwa pamoja kipindi hiki cha likizo.

Mpaka sasa tamasha hilo linaendelea huku wasanii Mbali Mbali wakiendelea kuishambulia 'Stage'. 

Msanii Rosa Ree akifanya yake jukwaani

Gigy Money akiwa jukwaani 

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil