Ismail Jussa
Hatua hiyo inakuja ikiwa Taifa lipo kwenye maombolezo ya siku 4 ya kuenzi vifo vilivyotokana na ajali ya kivuko cha Mv-Nyerere ambapo mpaka sasa bado vikosi vya ulinzi na usalama vinaendelea na zoezi la uokoaji wa miili.
Kupitia mtandao wake wa kijamii Jussa ameandika "Mhe. Hamad Masoud Hamad, Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa kutoka CUF, aliweka heshima kubwa alipokubali kuwajibika kisiasa baada ya ajali ya MV Spice Islanders na MV Skagit Zanzibar"
Septemba 10 mwaka 2011 ilikuwa ni siku ya majonzi makubwa visiwani Zanzibar baada ya meli ya Spice Islander kuzama katika eneo la Nungwi ikitokea Unguja kwenda Pemba na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 1,000.