Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kakobe amsaka aliyedaiwa 'kulala na Gwajima'

Jumatatu , 13th Mei , 2019

Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zacharia Kakobe amehoji juu ya kutoonekana kwa mwanamke anayedaiwa kufanya tendo la ndoa na Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima na kusema suala hilo lilikuwa na nia ovu.

Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima

Askofu Kakobe ametoa kauli hiyo jijini Dar es salaam wakati akizungumza kwenye ibada maalum iliyoandaliwa na Askofu Gwajima ambayo ililenga kuelezea kiundani zaidi kuhusiana kusambaa kwa video ya ngono inayomdhania kumuhusisha mtu anayefanana na Mchungaji huyo.

"Mshtaki wa Josephat Gwajima yuko wapi, ndiyo sasa hivi polisi wanahangaika kumtafuta amejificha mafichoni, sasa wewe una hoja ya kweli unajificha nini?, unachojificha ni nini wakati hii tuhuma umeihakikisha na unataka Gwajima ashughulikiwe, Yesu anauliza mshtaki wako Gwajima yuko wapi? mbaya zaidi nilivyoambiwa kwenye video hata sura ya mwanamke aliyetembea na Gwajima haonekani, sura yake imefichwa." amesema Kakobe.

"Kuna mwongozo ambao biblia unatutaka kuufuata yupo mchungaji mmoja ambaye tuhuma nyingi zilinifikia, kama Askofu Mkuu wakasema huyu anafanya uzinzi sana lakini kukawa hakuna ushahidi wanaoweza kuthibitisha, bila shaka nikawaambia mashtaka juu ya mzee hayawezi kukubalika nikawaambia watengeneze mtego, ili wamnase vizuri." ameongeza Kakobe.

"Walifanikiwa wakampata vizuri wakapiga picha nzuri za video na mnato, wakeleza mwanzo mpaka mwisho kiasi kwamba yule ambaye alishtakiwa alishindwa kujitetea na hapo ndipo tulipochukua hatua na yule tukamtenga kanisani, na kanisa langu wanajua hatuna mchezo katika hili". ameongeza Kakobe.

Mapema wiki iliyopita kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii, kulisambaa kipande cha video ambacho kilidaiwa kumuonesha Mchungaji Gwajima akifanya tendo la ndoa na mwanamke lakini Askofu Gwajima mwenyewe alikanusha taarifa hiyo na kueleza kuwa imelenga kumchafua kwa kuwa uchaguzi umekaribia.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa