Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kamanda Shana anusurika kutenguliwa, apewa onyo

Jumatatu , 22nd Jun , 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemuonya Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Jonathan Shana kutokana na kufanya mambo ambayo hayapo kwenye kazi yake.

Rais Magufuli na Kamanda Polisi mkoani Arusha, Jonathan Shana

Amesema hayo leo Juni 22, Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali wateule ambapo amesema kuwa ameamua kumsamehe Kamanda Shana pamoja na Afisa wa TAKUKURU mkoani humo lakini wasifanye makosa.

"IGP na Mkurugenzi wa TAKUKURU mko hapa, mkawaambie watendaji wenu walioko Arusha wafanye kazi nilizowatuma, nao leo nilikuwa niwatoe ambao ni RPC na Mkuu wa TAKUKURU wa Arusha", amesema Rais Magufuli.

"Nimeamua kuwasamehe lakini sijawasamehe moja kwa moja wakifanya kosa lolote wataondoka. Wakafanye kazi nilizowatuma wasifanye kazi wanazojituma wao, haiwezekani watu umewatuma kufanya kazi za serikali wanafanya kazi wanazozijua wao", ameongeza.

Katika tukio hilo, Rais Magufuli amemuapisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha mteule, Idd Kimanta pamoja na kushuhudia uapisho wa wakuu wawili wa wilaya ya Monduli, ACP Jotham Balele na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa.

Tazama tukio zima hapa.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali