Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kampeni ya Namthamini yaleta faraja Mbeya

Alhamisi , 3rd Oct , 2019

Kampeni ya Namthamini,  inayoratibiwa na East Africa Television na East Africa Radio yenye lengo la kumuwezesha mtoto wa kike asikose masomo shuleni akiwa katika hedhi, imeendelea kutoa msaada wa taulo za kike (Pedi) kwa shule mbalimbali  nchini ambapo awamu hii imefika Mbeya.

Baadhi ya wanafunzi na walimu mkoani Mbeya

Kampeni hiyo ya Namthamini imezifikia Shule tatu za Sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya  ambazo ni Nsenga, Stellafarm pamoja na Maziwa na kuzungumza na mabinti ambao walieleza changamoto zinazowakabili wanapokuwa kwenye hedhi na namna ambavyo taulo za kike zitawasaidia kuondokana na vikwazo wawapo shuleni.

Walimu wa shule zilizonufaika na msaada wa pedi  wameiomba EATV kuendelea kuzisaidia shule hizo, kwani uhitaji bado ni mkubwa.

Akizungumza kwa niaba ya Ofisa Elimu Sekondari Jiji la Mbeya, Hope Mariki amesema jumla ya Wanafunzi 379  wa kike kutoka Shule za Nsenga, Stellafarm na Maziwa wamenufaika na taulo hizo za kike.

Ni miaka mitatu sasa tangu East Africa Television na East Africa Radio, zianzishe  kampeni ya Namthamini yenye kauli mbiu isemayo Namthamini Nasimama Naye ambapo imefika katika mikoa mbalimbali nchini.

Kwa mwaka 2019 pekee tayari imefika katika mikoa ya Mbeya, Arusha, Dodoma, Tabora na Manyara na kugusa zaidi ya wanafunzi 5000.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa