Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kassim auawa na wasiojulikana shambani kwake

Alhamisi , 26th Jan , 2023

Mfanyabiashara mkoani Mwanza Yusuph Kassim, ameuawa na watu wasiojulikana shambani kwake, katika Kijiji cha Chabula wilayani Magu, baada ya kuvamiwa na watu hao akiwa na kijana wake wa kazi ambaye yeye alifanikiwa kuwatoroka watu hao.

Yusuph Kassim, aliyeuawa

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza Wilbroad Mutafungwa, amesema Jeshi la Polisi mkoani Mwanza limedhamiria kufanya upelelezi wa kina ili kubaini chanzo cha mauaji ya mfanyabiashara huyo.

Kamanda Mutafungwa amesema tarehe 23 ya mwezi huu majira ya usiku mfanyabiashara huyo akiwa shambani kwake na kijana aliyekuwa anamsaidia kazi shambani hapo ghafla wakatokea watu hao na kuwavamia huku kijana huyo akiwatoroka watu hao na kumuacha mfanyabishara huyo hadi kesho yake aliporudi na kuukuta mwili wa mfanyabiashra huyo ukiwa umelala pembeni ya bwawa ukiwa na jeraha kubwa kichwani.

"Marehemu alikuwa anatembelea shamba lake akiwa pamoja na kijana wake wa kazi anayefanya kazi ya kuangalia mifugo, usiku akavamiwa na watu watatu wanaume waliokuwa wameficha sura zao na vitambaa, walimshambulia kichwani kwa kutumia kitu chenye ncha kali, kijana wake alifanikiwa kuwatoroka watu hao na kukimbia ufukweni na kujificha," amesema Kamanda Mutafungwa.

Aidha Kamanda Mutafungwa amesema baada ya kupata taarifa ya tukio hilo polisi kwa kushirikiana na kitengo cha uchunguzi wa sayansi jinai walifika eneo la tukio na kuukagua mwili huo na kuuhifadhi katika hospitali ya wilaya ya Magu huku upelelezi wa tukio hilo ukiendelea hadi watuhumiwa watakapokamatwa.

HABARI ZAIDI

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea