Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kauli ya CHADEMA baada ya Mbowe kuitwa mlevi

Jumatano , 10th Jun , 2020

Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tumaini Makene amesema kuwa chama hicho hakiwezi kujibishana na wale wote waliotoa kauli za kwamba, Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe alilewa na kudondoka na si kushambuliwa kama chama kilivyosema.

Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa CHADEMA Tumaini Makene, na kulia ni Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Freeman Mbowe.

Hayo ameyabainisha leo Juni 10, 2020, wakati akizungumza kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio na kuongeza kuwa, wao ni hadhi ya juu hivyo wakisema wabishane nao watajishusha na kufanana nao, sababu kauli walizozitoa jana ndiyo zile zile walizozitoa Lissu aposhambuliwa kwa risasi.

"Ni vitu ambavyo mimi sikutaka kuvizungumza kwa sababu, ukizungumzia unajishusha kwenye level yao ya kufikiria, watu wengi wamewadharau na kuwapuuza, watu hao hao waliyoyazungumza maneno tunayoyasikia, ndiyo wale wale waliosema Lissu alijipiga risasi" amesema Makene.

Aidha Makene akizungumzia suala la kiongozi wa chama hicho kukosa walinzi, hali iliyopelekea kushambuliwa na watu wasiojulikana amesema kuwa, "Baada ya tukio la Lissu ilitungwa sheria ya vyama vya siasa, ambayo imepiga marufuku viongozi wa vyama vya siasa kujilinda, hilo swali inabidi muwaulize watawala wakati wanatunga sheria hii walijua litakalokuja kutokea baadaye?".
 

HABARI ZAIDI

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani