
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima na aibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Hamad Masauni
Naibu Katibu Mkuu huyo amefika kwenye hizo asubuhi ya leo Jumamosi Januari 01, 2020 ambapo anaungana na viongozi wengine waliwahi kuhojiwa na kwenye sakata hilo.
#HABARI Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima amehojiwa kwa takribani kwa saa 2 na dakika 55 katika ofisi za TAKUKURU - Dodoma, kuhusiana na tuhumu za viongozi wa wizara hiyo kuingia makubaliano kwa kusaini mkataba wa kununua vifaa vya zimamoto. pic.twitter.com/ff230Cl0g2
— East Africa Radio (@earadiofm) February 1, 2020
Wakati huohuo Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Hamad Masauni amefika ofisi hizo kwa ajili ya kuhojiwa majira ya saa 6 : 15 Mchana.
BREAKING NEWS : Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amefika ofisi za TAKUKURU Dodoma, ili kuhojiwa kutokana na madai ya viongozi wa wizara hiyo kusaini makubaliano ya zabuni ya kununua vifaa vya zimamoto na uokoaji vyenye thamani ya Shil. Tril. 1 kinyume na taratibu. pic.twitter.com/gzR88poZt2
— East Africa TV (@eastafricatv) February 1, 2020
Hivi karibuni kwenye sakata hili aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola alifika ofisini hapo kwa ajili ya kuhojiwa kwenye sakata hili.
anuari 23, 2020 Wakati wa uzinduzi wa nyumba za Askari Magereza Ukonga jijini Dar es salaam, Rais Magufuli aliagiza kuchunguzwa kwa sakata la kusainiwa kwa Mkataba wa zaidi ya Trilioni moja na kubainisha kuwa ulikuwa hauna nia njema kwa Watanzania.