Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kilimo,Viwanda vyapewa kipaumbele kampeni za urais

Jumatatu , 19th Oct , 2015

Zikiwa zimebaki siku 5 tu kufikia Oktoba 25 ambapo Uchaguzi Mkuu utafanyika kampeni za kugombea nafasi mbalimbali zimeendelea kushika kasi huku wagombea urais wakiendelea kutoa ahadi zaidi wakisisitiza kilimo na Viwanda.

Mgombea Urais kupitia chama cha CHAUMMA, Hashim Rungwe

Akiwa mkoa wa Mtwara mgombea urais kupitia chama cha CHAUMMA, Hashim Rungwe amesema kuwa endapo wananchi watampa ridhaa ya kuiongoza nchi basi katika sekta ya kilimo ataanzisha kilimo cha umwagiliaji kwa helkopta na ndege.

Awali, mgombea mwenza wa chama hicho, Issa Abasi Hussein, aliwataka wananchi hasa akina mama kuto shawishika na pesa kidogo kutoka kwa baadhi ya makada wa CCM ili kuwapa madaraka ya kuongoza kwa kipindi cha miaka mitano huku wao wakitaabika na hali ngumu ya maisha.

Akizungumza na mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara jijini Mbeya kwenye viwanja vya shule msingi Ruanda Nzovwe Mgombea Urais wa UKAWA kupitia CHADEMA, Edward Lowassa amesema kuwa akipata ridhaa ya watanzani Oktoba 25 mwaka huu Lowassa anaahidi kuunda serikali itakayofanya kazi kwa kasi ya "speed 120" kwa saa.

Lowassa amesisitiza kuwa endapo ataingia madarakani atahakikisha mpango wake wa kupandisha hadhi hospitali za wilaya kuwa za rufaa kwa kuboresha vitendea kazi na vifaa tiba.

Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye akautaka umma wa watanzania kumpigia kura mgombea wa UKAWA na kwamba ataibadilisha Tanzania kutoka kwenye umasikini.

Kwa upande wake Mgombea wa Chama cha Mapinduzi CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa jijini Mwanza wilayani Misungwi aliwaahidi wakazi wa jiji hilo kufufua viwanda vya pamba ili kukuza uchumi wa wakulima hao na nchi kwa Ujumla.

Aidha Dkt. Magufuli ameongeza kuwa katika serikali yake atahakikisha mawaziri atakaowachagua akiwemo waziri Mkuu lazima wawe wazalendo na kuwatumikia wananchi huku akiwaponda viongozi walitoka chama hicho na kuasisi na kuwaambia wananchi kuwa ccm haijafanya chochote.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali