
Kimbunga Ian hatimaye kimetua Marekani kikitokea Cuba huku kikiwa na upepo mkali unaofikia umbali wa kilomita 241 kwa saa.
Kimbunga hicho kimeleta uharibifu mkubwa ikiwemo kuharibu hosptali, magari na miti mikubwa kuanguka barabarani.
Wakazi wa Florida wameonywa kwamba saa 24 zijazo zitakua za hatari zaidi ambapo kunatarajiwa kutokea mvua kubwa na upepo mkali utakaodumu usiku kucha .
Kimbunga Ian kinatarajiwa kuelekea Kaskazini mwa Florida katika uwanja wa ndege wa Jacksonville ambao umesitisha safari zote za ndege.