Kimbunga hicho kiitwacho Nanmadol kinatarajiwa kuvuma kesho kikiwa na upepo mkubwa utakaovuma kwa kilomita 270 kwa saa huku mvua kubwa zikitarajiwa ndani ya saa 24 zijazo.
Tahadhari kutoka eneo la Kyushu, zinasema kwamba kutakua na maporomoko ya udogo na mafuriko makubwa, huku huduma za susafiri wa treni na ndege zikisitishwa.
Kyushu ni kisiwa kilichopo kusini mwa nchi hiyo kikiwa ni kisiwa kikubwa kati ya visiwa vinne ambavyo vinaunda Japan na kinakadiriwa kuwa na watu wanaofikia milioni 13.

