Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Leo sitaki kuongea habari ya Corona" - Waziri

Jumatano , 25th Mar , 2020

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, leo amekataa kuzungumzia wala kujibu maswali yaliyokuwa yakihoji kuhusu ugonjwa unaosababishwa na Virusi vya Corona na kwamba leo ilikuwa ni nafasi ya kuzungumzia masuala ya rasilimali watu katika sekta ya afya.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu

Waziri Ummy amekataa hii leo Machi 25, 2020, Jijini Dodoma, wakati akitoa taarifa ya nafasi 1,000 za ajira kwa madaktari zilizotolewa na Serikali, lengo likiwa ni kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za afya kwa wananchi.

"Leo sitaki kuongea habari ya Corona, mjiandae kesho tunaweza kukutana hapa saa 2:30 asubuhi, kwa sababu tusiharibu kikao hiki muhimu cha kuzungumzia rasilimali watu katika sekta ya afya ili kuweza kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za afya, bado wananchi wanaenda kwenye vituo vya afya wana Malaria, TB, HIV, Kisukari, Moyo na Saratani, Corona tutaongea kesho" amesema Waziri Ummy. 

Mpaka sasa idadi ya wagonjwa waliothibitika kuathirika na ugonjwa hatari wa mapafu na mafua makali, unaosababishwa na Virusi vya Corona hapa nchini ni 12.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali