Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

LHRC yamtaka Kikwete asitishe Bunge la Katiba

Jumatano , 17th Sep , 2014

Kituo cha Sheria na haki za bianadamu (LHRC) kimemtaka rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete kusitisha bunge maalumu la katiba badala ya kuendelea kusubiri mpaka ifikapo Oktoba 4 mwaka huu.

Rais wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.

Akiongea jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa maboresho na uwezeshaji wa LHRC Lulu Urio, amesema kuwa rais ana nafasi kikatiba kusimamisha Bunge la katiba, kuleta mwelekeo mpya wa mchakato wa katiba na kuleta maridhiano ya mapungufu yaliyoonekana hapo awali ambayo yaliondoa maridhiano baina ya wajumbe wa UKAWA na wajumbe wengine.

Hata hivyo Bi. Urio amesema ni vyema mwenyekiti wa Bunge la katiba akasitisha vikao vyake ili upatikane muafaka baina ya pande zote mbili zinazokinzana na kuongeza kuwa Rasimu ya katiba inatoa kipindi cha mpito cha miaka minne kabla ya kuanza kutumia katiba mpya.

Wakati huo huo, Makamu wa rais wa Tanzania Dk. Mohamed Gharib Bilal amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kutambua kuwa waandishi wa habari si adui hivyo basi wanapaswa kushirikiana nao.

Dk. Bilal ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua mkutano wa mashauriano kati ya Vyombo vya Habari na Vyombo vya Ulinzi, Usalama na Sheria ambao hata hivyo jeshi la polisi halikuweza kuleta mwakilishi wake kutokana na kukabiliwa na operesheni maalum.

Aidha Dkt. Balal amesema kuwa vyombo hivyo vielimishane kuhusu mipaka na maeneo ya ushirikiano ili kuondoa tofauti na mifarakano miongoni mwa vyombo hivyo ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa